Miaka mingi iliyopita, jemedari mkuu wa ufalme wa Mungu aliishi na kuanzisha Jeshi la wokovu. Alikuwa na viongozi wengi na alizaa matunda mengi kwa ajili ya ufalme wa Mungu. Siku moja, alituma ujumbe muhimu kwenda kwenye kundi la viongozi wake.
Aliomba kwamba kila mtu awepo ujumbe uwo unaposomwa. Viongozi walikusanyika pamoja, wakiulizana ujumbe muhimu ulihusu nini. Walipokuwa tayari, walifungua ujumbe uliyofungwa kwa lakiri na wakaisoma mbele ya kusanyiko. Walipatwa na mshtuko! Badala ya barua ndefu yenye maelekezo mengi, ujumbe huu muhimu ilikuwa na neno moja.
Neno hili lilikuwa lipi: “WENGINE”! Kusanyiko la viongozi wa Jeshi la wokovu walikaa pale wakiwa wameduwaa, wakijiuliza waufanyie nini ujumbe. “WENGINE”! William Booth alimaanisha nini kwa ujumbe huu usio wa kawaida? Walipokuwa wameketi pale wakiwa kimya wakitafakari kuhusu neno “WENGINE”, Nina uhakika Mungu alizungumza na kila mmoja wao..Neno “WENGINE” ni ujumbe kwa Wakristo wote.
Ujumbe wa “WENGINE”!
- Ujumbe wa “Wengine” ni; ‘WENGINE wanaishi”!
- Ujumbe wa “Wengine” ni; “Akili zetu lazime ziwekwa ajili ya ‘WENGINE”!
- Ujumbe wa “Wengine” ni; “Tuyatumie maisha yetu kwa ajlli ya ‘WENGINE”!
- Ujumbe wa “Wengine” ni; “Ni lazima tuishi kwa ajili ya ‘WENGINE”!
- Ujumbe wa “Wengine” ni: “Ni lazima tuwatumikie WENGINE”
- Ujumbe wa “Wengine” ni: “Lazima tuyatoe maisha yetu kwa ajlli ya WENGINE”
- Ujumbe wa “Wengine” ni; “Ni lazima tutumieBaraka zote tulizopewa na Mungu kwa ajili ya kuwasaidia “WENGINE”!
MAMBO MANNE AMBAYO NI LAZIMA UYAKUMBUKE KUHUSU “WENGINE”
Yapo mambo manne ambayo lazima uyazingatie linapokuja suala la“WENGINE”. Ukiyakumbuka mambo haya manne, utakuwa na mtazamo sahihi kuhusu wengine.
- WENGINE WANAMHITAJI KRISTO!
Daima kumbuka kwamba wapo watu wengi wanaomhitaji Kristo. Mamilioni na mamilioni ya watu hawamjui Yesu kwa sababu kanisa limeshindwa kuwaza kuhusu “wengine”. Wakristo wengi hawajali ukweli kuwa “wengine” hawamjui Kristo. Wana furaha ya kumfurahia Kristo katika makanisa na mikusanyiko yao. Tafadhali kumbuka kuwa, watu wengi sana hawajui kuhusu Kristo na wanasubiri kusikia injili safi ikihubiriwa. Wapo wengi ambao wangempa Mungu mioyo yao ikiwa mtu Fulani angewashuhudia. Hakika, “Wengine” wanamhitaji Kristo! Mwanamke wa Samaria aliwakumbuka “wengine” haraka. Baada ya kubarikiwa kwa kumjua Yesu, aliwakumbuka watu wote katika mji wake ambao hawakuwa wanajua kuhusu Yesu. Mwanamke wa Samari ni mfano mkuu wa mtu aliyewakumbuka “wengine”. Watu wengi hufurahi kupata kitu kizuri lakini ni nadra sana kufikiri kuhusu wengine wasio na kile walichonacho.
- WENGINE WANAHITAJI MCHUNGAJI!
“Kondoo wengine ninao!” Hii inamaanisha kuwa wapo kondoo wengine mahali pengine wanaomsubiri mchungaji. Kila mara Yesu alitambua uwepo wa watu wengine waliohitaji upendo na uangalizi wake. Yesu alitambua uwepo wa watu “wengine” wengi waliohitaji uangalizi na mafundisho yake ya kichungaji. Unawafahamu “wengine” wanaohitaji mchungaji na uangalizi wa kichungaji?
Ni muhimu kukumbuka kuwa Wakristo wengi wanahitaji mchungaji..Kuokoka ni jambo moja na kuangaliwa na kuchungwa kwa uangalifu ni jambo jingine.. Kuna uhitaji mkubwa wa waangalizi na wachungaji wazuri. Yesu alisema, “Kondoo wengine ninao”! Wapo Wakristo wengine wanaosubiri na kutumaini kuwa mchungaji atanyanyuliwa ilikuwaangalia na kuwalisha.Wakristo wengi huwafurahia watu wao wa Mungu wanaohudumu kwa upako. Hufurahia mahubiri mazuri na huduma kuu zinazowafikia kila siku Kwa sababu ya mambo mazuri wanayopata, husahau kuhusu wengine. Lakini wapo wengine wengi ambao wanamhitaji Mchungaji pia. Hebutufanye juhudi ya kuwainua wachungaji zaidi na kuwapeleka katika miji, majiji na vijiji vingi. “Wengine” wanahitaji wanahitaji makanisa! “Wengine” wachungaji! “Wengine” wanatusubiri tuwafunze!
- WENGINE LAZIMA WAUSIKIE UJUMBE!
Ikiwa Mungu amekubariki akakupa ujumbe mzuri, daima kumbuka kwamba wapo wengine ambao wanahitaji kuusikia ujumbe wako mzuri. Ni Baraka kwamba watu kama STEVEN WILLAR walisikia mzigo wa kuupeleka ujumbe wa imani kwa ulimwengu wote. Wengine wengi nje ya Marekani walihitaji kuusikia ujumbe wa imani. Nami ni mmoja wa “wengine”
walioupokea ujumbe mzuri wa Steven Willer. Steven Willer hakunifahamu lakini mimi ni mmoja wa “wengine” katika marupurupu waliofaidika kutokana na ujumbe wake. Hii ndiyo sababu nina mzigo wa kuupeleka kwa ulimwengu wote ujumbe wa uchungaji, kukua kwa kanisa na uaminifu kwa Mungu. Ikiwa Mungu amekubariki akakupa ujumbe mkuu, ni muhimu kwako kuwashirikisha wengine ujumbe huu watu wengi kadri inavyowezekana. Wengine wanahitaji kusikia! Wengine ni wa muhimu! Wengine lazima wausikie ujumbe!
- WENGINE WANA MATATIZO!
Usifikirie kuhusu matatizo yako. Fikiria kuhusu matatizo yanayoaathiri wengine. Watu wengi wana matatizo tofauti. Watu wengi wana matatizo magumu ambayo hawawezi kutatua. Mara nyingi tunakwamishwa na matatizo yetu wenyewe. Hatutazami juu kuona namna ambavyo wengine wanateseka. Inahuzunisha kwamba Wakristo wengi hawajikumbushi kuwa wengine wana matatizo. Ikiwa wewe, mwenye miguu miwili na macho mawili huwezi kupata kazi, ni vigumu namna gani kwa kipofu kupata kazi? Ikiwa wewe, mwenye miguu miwili na macho mawili huwezi kupata kazi, ni vigumu namna gani kwakiwete kupata kazi??
Ni wakati wa kuanza kufikiri kuhusu“wengine”! Ikoje kwa ombaomba? Ikoje kwa vipofu? Ikoje kwa mlemavu? Unapowaza kuhusu “wengine” utapata huruma na neema ya kuwasaidia!
Ubarikiwe sana mtu wa Mungu unaweza ku share ujumbe huu ili kuwafikia “WENGINE “
Ev.George Mwita.
Kwamawasiliano zaidi kwaajili ya Ushauri, Maswali, Maombi na maombezi, tuma ujumbe kupitia WhatsApp number.
0740444132/ 0782044449.